Wednesday, June 29, 2016

Usilie sababu kimeisha, tabasamu sababu kilitokea.



Dr Seuss ndiye aliyesema maneno hayo, nami nakazia tu hapo. Tumeumbwa na watu wanaotuzunguka tuishi pamoja tukisaidiana kwa  mambo mbalimbali. Katika kushirikiana katika kazi za kibinaadamu hutokea mengi kama vile kupata wenza na pengine kufika mbali nao kwa kuanzisha familia. 
Maisha ni matamu na yenye furaha tunapozungukwa na watu wenye furaha pia. Wao hutusaidia kujenga amani ndani yetu LAKINI, wanapoondoka sisi huumia sana kwani tunakosa ile furaha tuliyokuwa nayo japo kwa muda tu. 
Tunapofiwa ama kuondokewa na wapendwa wetu kwa sababu za kidunia mfano kusafiri, kuachana, kubadili mitazamo n.k, tunaumia kwani nasi ni binaadamu. Lakini kumbe hatupaswi kulia na kusononeka sababu kila kitu kina sababu. Naye Dr Seuss anatukumbusha hayo kwa kusema tutabasamu kwani walau tulikuwa nao, kutaishi na kufurahi pamoja.

Kuwa na mwanzo mpya. Jipe moyo upate amani kwa afya ya moyo wako. Tabasamu! Tabasamu! Tabasamu!

No comments:

Post a Comment