Monday, June 27, 2016

CABBAGE (KABEJI)



Kuna cabbage ya rangi ya kijani na ya damu ya mzee (maroon) ila inaitwa tu nyekundu
Leo tutaangalia faida za cabbage katika miili yetu. Kwanini tuile na inatufaidisha nini?

Mboga hii inatuhusu sana kama wanadamu. Ziangalie faida zifuatazo zitokanazo na ulaji wa kabeji:
  • Ziko za rangi tatu tofauti, kijani, nyeupe na nyekundu. Unanafasi kubwa ya kuchagua ni ya rangi ipi ule. Ya kijani ikikuchosha unakula nyekundu.
  • Haina kiwango kikubwa cha mafuta hivyo hainenepeshi ukiila sana; badala yake inakusaidia kuujenga mwili vizuri sababu ya nyuzi nyuzi zitokanazo na mboga hiyo.
  • Husaidia wajawazito katika kumlinda mtoto awapo tumboni pamoja na kukuza tumbo la mimba bila kuongeza mafuta. Hapo hapo ni chanzo cha folate ambacho ni kipengele kimoja wapo cha DNA (deoxyribonucleic acid-husaidia ugunduzi wa kirithi kwa mwanadamu katika seli (cell) karibuni zote katika mwili); hivyo, huleta uhusiano mzuri wa mama na mtoto.
  • Huipa mifupa na mwili nguvu sababu ya Vitamin C inayoupa mwili nguvu kujiepusha na magonjwa kwa haraka na Vitamin K ambazo husaidia katika kuleta nguvu kwenye mifupa hivyo kusababisha isilegee ama kujikunja. 
  • Inamadini kama Calcium, Potasium, Phosphorus, Manganese, Iron na Magnesium ambayo husaidia kiwango cha moyo na presha ya damu. 
  • Madini ya chuma (Iron) ni muhimu sana sababu huleta chembe chembe nyekundu za damu ambazo husaidia wakina mama wajawazito kutokuwa na upungufu wa damu. 
  • Ni mboga ya msimu. Haivunwi mara kwa mara hivyo inapopatikana ile kwa wingi kabla hujaikosa isipokuwepo.

  • Kabeji nyekundu husaidia kuzuia kansa kwa kuachisha ukuaji/uzalishaji wa seli za cancer.
Kikombe kimoja cha kabeji nyekundu kina 33% ya Vitamin A ambazo tunapaswa kula kila siku.
EMBU ANDAA KABEJI YAKO SASA...

*Waweza iunga kwa kitunguu pekee.
*Waweza ikaanga na chumvi.
*Waweza iunga na kitunguu na nyanya.
*Waweza ipika kwa viungo vyote yaani nyanya, kitunguu, karoti, hoho, pilipili na mazaga mengine unayoyafahamu.
*Waweza ipika kwa karanga au nazi.
*Wengine hupendelea kuiweka kwenye kachumbari. 
*Wale wa diet, inachemswa bila mafuta wala chumvi...kazi kwako!!

No comments:

Post a Comment