Monday, June 20, 2016

Courage isn't having the strength to go on, it is going on when you don't have strength...



Napoleon ndiye aliyesema maneno haya " Ujasiri sio kuwa na nguvu za kusonga mbele ila ni kusonga mbele bila ya kuwa na  nguvu".

Binadamu tunakumbwa na changamoto nyingi sana. Wakati mwingine tunapata shida zinazofururiza mpaka tunajiuliza kama Mungu yupo; tukidhani kumetelekezwa njiani. Napoleon anatukumbusha kuwa na nguvu hasa pale tunapokata tamaa kabisa, kwa kufanya hivyo tutakuwa jasiri. Ewe ndugu, usikate tamaa leo. Onyesha ujasiri wako kwa kusonga mbele hata kama unahisi kuelemewa na mizigo ya dunia. Onyesha ujasiri wako hata kama rafiki zako wote wamekukimbia. Onyesha ujasiri kwa kujikongoja bila kuwa na nguvu kwani ni kwa kufanya hivyo, nguvu zitajitengeneza ndani yako na utafanya mambo makubwa mpaka ujishangae. Kuwa jasiri leo...

No comments:

Post a Comment