Tuesday, June 14, 2016

JINSI YA KUPIKA FUTARI YA MIHOGO NA SAMAKI


MAHITAJI:
  • Mihogo
  • Nazi
  • Chumvi
  • Samaki
  • Limao/ndimu
  • Mafuta

*Pilipili manga
*Kitunguu swaumu
*Tangawizi

JINSI YA KUPIKA:
  • Mihogo

Menya mihogo
Kata kata vipande vidogo vidogo
Bandika jikoni
Acha kwenye moto kwa dakika kumi kama unatumia gesi
Andaa nazi
Mimina nazi kwenye mihogo ikiwa bado inachemka
Tia chumvi kidogo
Acha vitokote kwa dakika kumi nyingine ili nazi ichemke
Bonyeza kwa mwiko uone kama imelainika 
Kama imelainika epua, kama bado ongeza maji kidogo ili iive

  • Samaki

Andaa samaki wako kwa kuwaparua na kuwaosha vizuri
Wakate msitari kila upande
Pakaa chumvi na limao/ndimu
Pakaa viungo vingine kama pilipili manga, swaumu na tangawizi (ukipenda)
Weka mafuta kwenye kikaangio
Injika mafuta kwenye moto yachemke
Kaanga samaki mpaka wawe na rangi ya kahawia
Epua

Waweza kuipamba sahani uliyopakulia chakula chako kwa kachumbari na limao/ndimu kwa ajili ya kuongeza ladha zaidi wakati wa kula.

Nakutakia mlo mwema....

No comments:

Post a Comment