Monday, June 20, 2016

JINSI YA KUPIKA VIAZI MBATATA, NYAMA YA KUSAGWA NA UJI WA MUHOGO

MAHITAJI
  • Viazi mbatata (viazi ulaya)
  • Nyama ya kusagwa
  • Unga wa muhogo
  • Nyanya
  • Vitunguu
  • Pili pili hoho
  • Karoti
  • Mafuta ya kupikia
  • Maji safi
  • Chumvi
  • Ndimu
  • Pili pili mtama 
  • Ukwaju

MAANDALIZI



  • Menya viazi
  • Kata size unayotaka ama viache vikiwa vizima
  • Vioshe vizuri kwa maji safi
  • Andaa nyanya, vitunguu, hoho na karoti
  • Saga nyama (kama ulinunua ambayo haijasagwa)
  • Kamua ndimu kwenye chombo kidogo
  • Pekecha ukwaju kama unavyotengeneza juisi yake kisha chuja

JINSI YA KUPIKA
*Viazi vya nyama




  • Washa jiko lako
  • Injika sufuria la kupikia jikoni
  • Weka mafuta kwenye sufuria la kupikia
  • Mafuta yakichemka mwaga vitunguu na geuza viive
  • Weka ziazi mbatata kwenye mchanganyiko wako
  • Koroga kwa muda wa dakika kama kumi hivi, mpaka viungulie
  • Tia nyanya na funika ichemke haraka
  • Baada ya dakika moja, funua na geuza
  • Weka nyama ikiwa bado mbichi
  • Nyunyiza mchuzi wa ndimu uliyoisha kamua ili kutoa harufu ya shombo ya ubichi wa nyama
  • Geuza geuza mchanganyiko wako uchanganyike vizuri
  • Acha vichemke kwa dakika kama tano kisha geuza tena
  • Weka hoho na karoti kwa pamoja kisha funika
  • Baada ya dakika tano (kwa moto mdogo usiounguza), funua na koroga vichanganyike vizuri
  • Epua


  • *Uji
    • Bandika maji
    • Acha yachemke yawe vuguvugu
    • Koroga unga kiasi kwenye chombo chenye maji (kama unavyokoroga ugali)
    • Mwaga mchanganyiko ndani ya maji yanayochemka jikoni
    • Acha vichemke kama unavyopika ugali
    • Vikiisha kuchemka, weka ukwaju kidogo kuleta ladha (ikizidi inakuwa chachu)
    • Weka sukari iivie (pima kulingana na uji uliopika
    • Malizia kwa kuweka pilipili mtama kidogo



    Mlo mwema...

    No comments:

    Post a Comment