Monday, July 4, 2016

Unaweza kushindwa kudhibiti tabia hasi za mtu. Lakini unaweza kudhibiti muda gani unashiriki ndani yake.


Toka upate ufahamu wa kunyambua mambo, leo hii jiulize umeachana na wangapi? Jana ulikuwa na rafiki huyu lakini leo uko na mwingine. Uwezo wa kuwa na mwingine ndio unaoonesha ujasiri wako kwani hukutaka kuvumilia kuwa na mtu ambaye hana nia nzuri na wewe ama faida katika maisha yako.

Binadamu tunatofautiana sana. Haiwezekani ukakutana na mtu ambaye utafanana naye kila kitu lakini unaweza kuwa na mtu au watu ambao mtakuwa na tabia japo chache zinazorandana. Unapokutana na mtu au watu msiowezana hasa kitabia muache mara moja asijekukuumiza kichwa. Jinsi unavyoendelea kubaki naye ndivyo utakavyokwazika ama kuteseka. 

Haijalishi anakupa pesa kiasi gani, mali za thamani, utambulisho kwa watu wazito/vigogo. Kama hakupi furaha, hakuonyeshi upendo, hana muda ma wewe basi fanya hima uachane naye. Tunaishi mara moja, usivumilie ukidhani utabahatika kuwa na "part two" kuishi...mkimbie. Fikiria mara mbili kisha fanya maamuzi sahihi na ya haraka. Unaweza...

No comments:

Post a Comment