Thursday, June 16, 2016

Fanya kazi kwa bidii, kuwa na furaha, na tengeneza historia


Anaitwa Jeff, anasema fanya kazi kwa bidii...lakini si kazi tu, furahi pia na anamalizia kwa kusema tengeneza historia.
Toka uzaliwe, ni nini umefanya kutengeneza historia? Umefikiria ni nini utaacha kama kumbukumbu ukifa leo?!? Watu wengi wanaaga dunia lakini wachache wanakumbukwa na ulimwengu huku wengine wakikumbukwa na familia zao tu. Kufanya kazi ni wajibu wa kila mtu lakini hakikisha unafurahia kazi uifanyayo ili iwasaidie wengi zaidi ya wewe pekee (oneself). Kwa kufanya hivyo utajenga ukuta imara kati yako na wanaokuzunguka na pengine zaidi za hapo kwa kuujumlisha ulimwengu. TENGENEZA HISTORIA SASA....

No comments:

Post a Comment