Endelea kukimbia hata kama ni wa mwisho katika mashindano. Huwezi jua, yawezekama ukawa bingwa.
Ninawakummbusha ndugu zanguni kutokata tamaa maana muda unaokata tamaa unaweza kuwa ndio muda sahihi kabisa kwa wewe kupata mafanikio/ ukitakacho/ ulichoomba kwa muda mrefu/ kufikia ndoto zako na kadhalika.
Ukihisi kuacha usiache, kazana kwa kuwa umekaribia. Sote ni washindi kwa muda tofauti na kwa namna tofauti.
Wewe ni wa muhimu hivyo jijali muda wote. Zingatia lishe bora na uchangamshe mwili wako kwa mazoezi kiasi. Furahi, afya ya akili huupa mwili afya pia. J. A. Y!!
Showing posts with label MSEMO WA SIKU. Show all posts
Showing posts with label MSEMO WA SIKU. Show all posts
Friday, July 22, 2016
Thursday, July 21, 2016
Kila lililokamilika huanza kwa uamuzi wa kujaribu.
Msemo wa leo ni wa kutuhamasisha zaidi. Kila lililokamilika huanza kwa uamuzi wa kujaribu.
Chukua mfano huu mdogo. Umekaa kochini ukatamani maji ya kunywa lakini unaona uvivu kunyanyuka, hutapata maji. Kuna watu ndani unashindwa kuwaomba msaada wakuletee, hutapata maji. Umepata ila ni ya moto unahitaji ya baridi na huchukui uamuzi wowote, hutakata kiu yako.
Sasa, unataka kufanikisha mipango yako ambayo pengine hujaanza hata kujipanga, hutaikamilisha. Inatakiwa ifikie wakati ambapo utasimama hata kama umechoka au hujiwezi kufedha au kimwili. Anza safari huku ukiomuomba Mungu, naye atakuimarisha ukiwa njiani na utafika salama.
Fanya maamuzi haraka ya wapi uanze ama wapi upite na sio maamuzi ya kuendelea kusubiri. Bora ujaribu ushindwe kuliko usijaribu kumbe unajikosesha faida. Na ukijaribu ukashindwa usikate tamaa haraka, jaribu tena na tena mpaka utakapoona haiwezekani kabisa; ingawaje hakuna lisilowezekana kwa Mungu. Utachelewa lakini sio kushindwa.
Kazi kwako...
Friday, July 8, 2016
KUWA MTU MZURI LAKINI USIPOTEZE MUDA KUTHIBITISHA
Tumeumbwa tupendane lakini haimaanishi umpende kila mmoja sawa sawa. Tunapaswa kusaidiana na kuheshimiana lakini inaposhindikana unaacha. Usiumize kichwa kumfurahisha asiyetaka au asiyestahili. Kakupotezea muache, usimlete karibu kilazima.
Asipokuona mzuri machoni mwake muache sababu wapo wengine maelfu zaidi wanaokuona uko sawa. Hajaona thamani yako muache sababu wapo wengi zaidi wanaotambua uwepo wako na hasa umuhimu wako.
Timiza wajibu wako kwa kila mmoja katika jamii yako kulingana na nafasi yako kwao. Jali, heshimu, penda, sahihisha, funisha, ongoza, furahisha, onya, lakini kama haionekani kumsaidia unayemfanyia badilisha njia, mtazamo, suluhisho, matendo. Usilazimishe wala kung'ang'ania, utajiumiza.
Yamkini mia wakakusema vibaya, usiumie sababu yupo japo mmoja anayetambua uzuri wako kwa wema wako; na hilo ni kuu mno. Kuwa hivyo ulivyo na uache mengineyo yapite njia yake...
Monday, July 4, 2016
Unaweza kushindwa kudhibiti tabia hasi za mtu. Lakini unaweza kudhibiti muda gani unashiriki ndani yake.
Toka upate ufahamu wa kunyambua mambo, leo hii jiulize umeachana na wangapi? Jana ulikuwa na rafiki huyu lakini leo uko na mwingine. Uwezo wa kuwa na mwingine ndio unaoonesha ujasiri wako kwani hukutaka kuvumilia kuwa na mtu ambaye hana nia nzuri na wewe ama faida katika maisha yako.
Binadamu tunatofautiana sana. Haiwezekani ukakutana na mtu ambaye utafanana naye kila kitu lakini unaweza kuwa na mtu au watu ambao mtakuwa na tabia japo chache zinazorandana. Unapokutana na mtu au watu msiowezana hasa kitabia muache mara moja asijekukuumiza kichwa. Jinsi unavyoendelea kubaki naye ndivyo utakavyokwazika ama kuteseka.
Haijalishi anakupa pesa kiasi gani, mali za thamani, utambulisho kwa watu wazito/vigogo. Kama hakupi furaha, hakuonyeshi upendo, hana muda ma wewe basi fanya hima uachane naye. Tunaishi mara moja, usivumilie ukidhani utabahatika kuwa na "part two" kuishi...mkimbie. Fikiria mara mbili kisha fanya maamuzi sahihi na ya haraka. Unaweza...
Wednesday, June 29, 2016
Usilie sababu kimeisha, tabasamu sababu kilitokea.
Dr Seuss ndiye aliyesema maneno hayo, nami nakazia tu hapo. Tumeumbwa na watu wanaotuzunguka tuishi pamoja tukisaidiana kwa mambo mbalimbali. Katika kushirikiana katika kazi za kibinaadamu hutokea mengi kama vile kupata wenza na pengine kufika mbali nao kwa kuanzisha familia.
Maisha ni matamu na yenye furaha tunapozungukwa na watu wenye furaha pia. Wao hutusaidia kujenga amani ndani yetu LAKINI, wanapoondoka sisi huumia sana kwani tunakosa ile furaha tuliyokuwa nayo japo kwa muda tu.
Tunapofiwa ama kuondokewa na wapendwa wetu kwa sababu za kidunia mfano kusafiri, kuachana, kubadili mitazamo n.k, tunaumia kwani nasi ni binaadamu. Lakini kumbe hatupaswi kulia na kusononeka sababu kila kitu kina sababu. Naye Dr Seuss anatukumbusha hayo kwa kusema tutabasamu kwani walau tulikuwa nao, kutaishi na kufurahi pamoja.
Kuwa na mwanzo mpya. Jipe moyo upate amani kwa afya ya moyo wako. Tabasamu! Tabasamu! Tabasamu!
Thursday, June 23, 2016
LAKINI SOTE TUNAOGOPA KUSEMA VILIVYO NA THAMANI KUSEMWA...
Hofu ya mwanadamu hutofautiana kwa ukuu. Lakini sote huogopa kwa namna fulani. Hata mwenye nguvu huhofia wenzao wenye.
Tuogope yote lakini tusiogope kusema ukweli inapobidi, na si ukweli tu ila kuzungumza kwa ujumla.
Wapo wenye mawazo mazuri sana ambayo yasipokaliwa kimya yanaweza kuleta athari kubwa tu kwa mtu mmoja au jamii nzima.
Yamkini ukambadilisha mtu / watu, ukaokoa maisha ya mtu / watu, ukapata msaada ulioukusudia au kuutamani kwa muda mrefu, ukatambulika katika familia, ukoo, eneo, nchi, bara au dunia kwa kusema kwako.
Usisite, usikate tamaa, usiogope kusema sababu yule ni mtu mzima, yule ni mkali, yule ni mpole sana, yule haeleweki, yule simuamini. Usihisi labda hivi, labda vile. Sema usikike hata kama utamkwaza, hata kama utamuudhi, hata kama atakujibu vibaya, atakukaripia, atakutukana ama atakukalia kimya. Katika yote, hakika kuna ambalo litamgusa na kumbadilisha japo kidogo.
Kama ni cha thamani kiseme...kitaleta mabadiliko!! Kiseme, moyo wako uridhike pia!!
Katika sehemu ya tatu, kifungu cha 18 cha Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977, tunaona kuwa kila mwanadamu anauhuru wa kuongea / kuzungumza. Kumbe basi, ni wajibu wa kila mmoja kuzungumza kile anachoona ni sahihi, ilimradi tu asiseme uongo wala kuzusha jambo.
Usiogope!!
Monday, June 20, 2016
Courage isn't having the strength to go on, it is going on when you don't have strength...
Napoleon ndiye aliyesema maneno haya " Ujasiri sio kuwa na nguvu za kusonga mbele ila ni kusonga mbele bila ya kuwa na nguvu".
Binadamu tunakumbwa na changamoto nyingi sana. Wakati mwingine tunapata shida zinazofururiza mpaka tunajiuliza kama Mungu yupo; tukidhani kumetelekezwa njiani. Napoleon anatukumbusha kuwa na nguvu hasa pale tunapokata tamaa kabisa, kwa kufanya hivyo tutakuwa jasiri. Ewe ndugu, usikate tamaa leo. Onyesha ujasiri wako kwa kusonga mbele hata kama unahisi kuelemewa na mizigo ya dunia. Onyesha ujasiri wako hata kama rafiki zako wote wamekukimbia. Onyesha ujasiri kwa kujikongoja bila kuwa na nguvu kwani ni kwa kufanya hivyo, nguvu zitajitengeneza ndani yako na utafanya mambo makubwa mpaka ujishangae. Kuwa jasiri leo...
Thursday, June 16, 2016
Fanya kazi kwa bidii, kuwa na furaha, na tengeneza historia
Anaitwa Jeff, anasema fanya kazi kwa bidii...lakini si kazi tu, furahi pia na anamalizia kwa kusema tengeneza historia.
Toka uzaliwe, ni nini umefanya kutengeneza historia? Umefikiria ni nini utaacha kama kumbukumbu ukifa leo?!? Watu wengi wanaaga dunia lakini wachache wanakumbukwa na ulimwengu huku wengine wakikumbukwa na familia zao tu. Kufanya kazi ni wajibu wa kila mtu lakini hakikisha unafurahia kazi uifanyayo ili iwasaidie wengi zaidi ya wewe pekee (oneself). Kwa kufanya hivyo utajenga ukuta imara kati yako na wanaokuzunguka na pengine zaidi za hapo kwa kuujumlisha ulimwengu. TENGENEZA HISTORIA SASA....
Wednesday, June 15, 2016
Maisha ya baadaye mali ya yule anayejiandaa leo.
The Future belongs to those who prepare for it......
Haya ni maneno ya mwanahistoria mmoja anayefahamika kwa jina la Malcom X.
Ndugu, ukitaka maisha mazuri ya baadaye sharti ujiandae leo hii. Anza leo, usingoje kesho usiyokuwa na uhakika nayo. Watu wengi hupenda kusubiria kupata mtaji kamili ndipo waanze biashara. wengine husubiri wapate mtoto ndipo wajifunze kulea. wengine wanasubiri mitihani ikaribie ndipo waanze kusoma, wengine wanasubiri shida ndipo wamkumbuke Mungu, wengine hutaka kupunguza miili yao kwa afya njema lakini wanasema "nitaanza kesho au mwezi ujao au tarehe moja (nayo haifiki)". Tusiwe watu wa kusubiri....tuanze sasa. Chochote ulichonacho kiwe kingi au kidogo, anza nacho. UKITAKA MAZURI YA BAADAYE SHARTI UJIANDAE MAPEMA.
Subscribe to:
Posts (Atom)








