Wednesday, June 15, 2016

Maisha ya baadaye mali ya yule anayejiandaa leo.

The Future belongs to those who prepare for it......

Haya ni maneno ya mwanahistoria mmoja anayefahamika kwa jina la Malcom X.


Ndugu, ukitaka maisha mazuri ya baadaye sharti ujiandae leo hii. Anza leo, usingoje kesho usiyokuwa na uhakika nayo. Watu wengi hupenda kusubiria kupata mtaji kamili ndipo waanze biashara. wengine husubiri wapate mtoto ndipo wajifunze kulea. wengine wanasubiri mitihani ikaribie ndipo waanze kusoma, wengine wanasubiri shida ndipo wamkumbuke Mungu, wengine hutaka kupunguza miili yao kwa afya njema lakini wanasema "nitaanza kesho au mwezi ujao au tarehe moja (nayo haifiki)". Tusiwe watu wa kusubiri....tuanze sasa. Chochote ulichonacho kiwe kingi au kidogo, anza nacho. UKITAKA MAZURI YA BAADAYE SHARTI UJIANDAE MAPEMA.

No comments:

Post a Comment