Thursday, June 23, 2016

JINSI YA KUPIKA KATLESI


MAHITAJI
  • Viazi ulaya
  • Nyama ya kusagwa
  • Kitunguu swaumu
  • Kitunguu maji
  • Hoho
  • Karoti
  • Mafuta ya kupikia
  • Mayai
  • Pilipili (ukitaka)
MAANDALIZI
  • Menya viazi
  • Vioshe na maji safi
  • Menya na twanga kitunguu swaumu
  • Katakata viungo vipande vidogo vidogo
  • Pasua majai weka kwenye chombo kisafi kisha koroga na chumvi kwa mbali
MAPISHI
  • Chemcha viazi viive
  • Twanga au ponda ponda vilainike
  • Chemsha nyama na chumvi kwa mbali
  • Ikiishaiva weka kitunguu swaumu, kitunguu maji, hoho, karoti na pilipili ukitaka
  • Changanya viungo vyako kwa pamoja vichanganyike vizuri (hakikisha hakuna maji bali mvuke)
  • Weka viazi ulivyoisha viponda
  • Changanya vyote kwa pamoja
  • Chukua kidogo kidogo mkononi
  • Finyanga kwa urefu
zikiwa tayari kwa kukaangwa
  • Tosa kwenye mayai
  • Kaanga kwenye mafuta ya moto
zimeiva, tayari kwa kuliwa
Karibu mezani...




No comments:

Post a Comment