Wednesday, June 22, 2016

JINSI YA KUPIKA TAMBI ZA KUKAANGWA NA MAINI ROSTI



MAHITAJI
  • Maini
  • Tambi
  • Viazi ulaya
  • Nyanya
  • Kitunguu
  • Karoti
  • Hoho
  • Ndimu
  • Kitunguu swaumu
  • Chumvi
  • Mafuta ya kupikia
  • Sukari
  • Iriki
  • Maji safi
MAANDALIZI
  • Kata maini kwa shepu unayotaka
  • Menya viazi kisha kata kata shepu ya maboksi
  • Osha maini na viazi kwa maji safi
  • Katakata viungo vya kupikia (nyanya, kitunguu, hoho na karoti)
  • Menya vitunguu swaumu kisha twangaa vilainike
  • Menya kisha twanga iriki kama punje tano au sita


JINSI YA KUPIKA
*Maini
  • Chemsha maini kidogo kwa maji uliyooshea
  • Weka chumvi na ndimu kidogo kuleta ladha
  • Maji yakiisha kaukia unaweka pembeni kwenye chombo kingine
  • Weka mafuta kiasi ya kupikia
  • Mafuta yakishachemka unaweka kitunguu mpaka kiwe na rangi ya kahawia
  • Weka nyanya
  • Kaanga kaanga nyanya mpaka ziwe rojorojo
  • Weka viazi kisha geuza geuza
  • Weka kitunguu swaumu 
  • Weka maini uliyoyachemsha


  • Koroga koroga mpaka uone maini yanataka kushikana
  • Weka maji kipimo ukitakacho (ila kwa rosti, weka maji kidogo tu kama nusu kikombe cha chai)
  • Vikiishachemka, unaweka karoti na hoho mwishoni
  • Funika vichemke
  • Baada ya muda kidogo unageuza kisha angalia kama chumvi iko sawa (kama bado unaongeza kidogo kabla ya kuipua)
  • Maini yatakuwa tayari kwa kuliwa
*Tambi
  • Chemsha maji yatokote
  • Weka mafuta  kwenye sufuria motoni
  • Yakiishapata moto, vunja vunja tambi kisha ziweke kwenye mafuta
  • Rusha rusha sufuria kuzigeuza mpaka zibadilike rangi kuwa kahawia (brown)
Tambi baada ya kukaangwa (hazijawekwa maji)
  • Weka maji ya moto yafikie juu kidogo ya tambi zinapoishia kwenye sufuria
  • Weka sukari kidogo na iriki uliyoisha itwanga
  • Funika vichemke
  • Angalia angalia kama zimeiva
  • Maji yakikaribia kuisha unatoa sufuria motoni.





Chakula tayari...
Maji mengi huleta mchuzi
Tambi baada ya kuiva



Rosti (haina mchuzi)
Enjoy!!

No comments:

Post a Comment