Thursday, July 21, 2016

Kila lililokamilika huanza kwa uamuzi wa kujaribu.


Msemo wa leo ni wa kutuhamasisha zaidi. Kila lililokamilika huanza kwa uamuzi wa kujaribu.

Chukua mfano huu mdogo. Umekaa kochini ukatamani maji ya kunywa lakini unaona uvivu kunyanyuka, hutapata maji. Kuna watu ndani unashindwa kuwaomba msaada wakuletee, hutapata maji. Umepata ila ni ya moto unahitaji ya baridi na huchukui uamuzi wowote, hutakata kiu yako.

Sasa, unataka kufanikisha mipango yako ambayo pengine hujaanza hata kujipanga, hutaikamilisha. Inatakiwa ifikie wakati ambapo utasimama hata kama umechoka au hujiwezi kufedha au kimwili. Anza safari huku ukiomuomba Mungu, naye atakuimarisha ukiwa njiani na utafika salama.

Fanya maamuzi haraka ya wapi uanze ama wapi upite na sio maamuzi ya kuendelea kusubiri. Bora ujaribu ushindwe kuliko usijaribu kumbe unajikosesha faida. Na ukijaribu ukashindwa usikate tamaa haraka, jaribu tena na tena mpaka utakapoona haiwezekani kabisa; ingawaje hakuna lisilowezekana kwa Mungu. Utachelewa lakini sio kushindwa.

Kazi kwako...

No comments:

Post a Comment