Friday, July 8, 2016

KUWA MTU MZURI LAKINI USIPOTEZE MUDA KUTHIBITISHA




Tumeumbwa tupendane lakini haimaanishi umpende kila mmoja sawa sawa. Tunapaswa kusaidiana na kuheshimiana lakini inaposhindikana unaacha. Usiumize kichwa kumfurahisha asiyetaka au asiyestahili. Kakupotezea muache, usimlete karibu kilazima.

Asipokuona mzuri machoni mwake muache sababu wapo wengine maelfu zaidi wanaokuona uko sawa. Hajaona thamani yako muache sababu wapo wengi zaidi wanaotambua uwepo wako na hasa umuhimu wako. 

Timiza wajibu wako kwa kila mmoja katika jamii yako kulingana na nafasi yako kwao. Jali, heshimu, penda, sahihisha, funisha, ongoza, furahisha, onya, lakini kama haionekani kumsaidia unayemfanyia badilisha njia, mtazamo, suluhisho, matendo. Usilazimishe wala kung'ang'ania, utajiumiza.

Yamkini mia wakakusema vibaya, usiumie sababu yupo japo mmoja anayetambua uzuri wako kwa wema wako; na hilo ni kuu mno. Kuwa hivyo ulivyo na uache mengineyo yapite njia yake... 

No comments:

Post a Comment