Monday, June 20, 2016

Courage isn't having the strength to go on, it is going on when you don't have strength...



Napoleon ndiye aliyesema maneno haya " Ujasiri sio kuwa na nguvu za kusonga mbele ila ni kusonga mbele bila ya kuwa na  nguvu".

Binadamu tunakumbwa na changamoto nyingi sana. Wakati mwingine tunapata shida zinazofururiza mpaka tunajiuliza kama Mungu yupo; tukidhani kumetelekezwa njiani. Napoleon anatukumbusha kuwa na nguvu hasa pale tunapokata tamaa kabisa, kwa kufanya hivyo tutakuwa jasiri. Ewe ndugu, usikate tamaa leo. Onyesha ujasiri wako kwa kusonga mbele hata kama unahisi kuelemewa na mizigo ya dunia. Onyesha ujasiri wako hata kama rafiki zako wote wamekukimbia. Onyesha ujasiri kwa kujikongoja bila kuwa na nguvu kwani ni kwa kufanya hivyo, nguvu zitajitengeneza ndani yako na utafanya mambo makubwa mpaka ujishangae. Kuwa jasiri leo...

JINSI YA KUPIKA VIAZI MBATATA, NYAMA YA KUSAGWA NA UJI WA MUHOGO

MAHITAJI
  • Viazi mbatata (viazi ulaya)
  • Nyama ya kusagwa
  • Unga wa muhogo
  • Nyanya
  • Vitunguu
  • Pili pili hoho
  • Karoti
  • Mafuta ya kupikia
  • Maji safi
  • Chumvi
  • Ndimu
  • Pili pili mtama 
  • Ukwaju

MAANDALIZI



  • Menya viazi
  • Kata size unayotaka ama viache vikiwa vizima
  • Vioshe vizuri kwa maji safi
  • Andaa nyanya, vitunguu, hoho na karoti
  • Saga nyama (kama ulinunua ambayo haijasagwa)
  • Kamua ndimu kwenye chombo kidogo
  • Pekecha ukwaju kama unavyotengeneza juisi yake kisha chuja

JINSI YA KUPIKA
*Viazi vya nyama




  • Washa jiko lako
  • Injika sufuria la kupikia jikoni
  • Weka mafuta kwenye sufuria la kupikia
  • Mafuta yakichemka mwaga vitunguu na geuza viive
  • Weka ziazi mbatata kwenye mchanganyiko wako
  • Koroga kwa muda wa dakika kama kumi hivi, mpaka viungulie
  • Tia nyanya na funika ichemke haraka
  • Baada ya dakika moja, funua na geuza
  • Weka nyama ikiwa bado mbichi
  • Nyunyiza mchuzi wa ndimu uliyoisha kamua ili kutoa harufu ya shombo ya ubichi wa nyama
  • Geuza geuza mchanganyiko wako uchanganyike vizuri
  • Acha vichemke kwa dakika kama tano kisha geuza tena
  • Weka hoho na karoti kwa pamoja kisha funika
  • Baada ya dakika tano (kwa moto mdogo usiounguza), funua na koroga vichanganyike vizuri
  • Epua


  • *Uji
    • Bandika maji
    • Acha yachemke yawe vuguvugu
    • Koroga unga kiasi kwenye chombo chenye maji (kama unavyokoroga ugali)
    • Mwaga mchanganyiko ndani ya maji yanayochemka jikoni
    • Acha vichemke kama unavyopika ugali
    • Vikiisha kuchemka, weka ukwaju kidogo kuleta ladha (ikizidi inakuwa chachu)
    • Weka sukari iivie (pima kulingana na uji uliopika
    • Malizia kwa kuweka pilipili mtama kidogo



    Mlo mwema...

    Thursday, June 16, 2016

    Fanya kazi kwa bidii, kuwa na furaha, na tengeneza historia


    Anaitwa Jeff, anasema fanya kazi kwa bidii...lakini si kazi tu, furahi pia na anamalizia kwa kusema tengeneza historia.
    Toka uzaliwe, ni nini umefanya kutengeneza historia? Umefikiria ni nini utaacha kama kumbukumbu ukifa leo?!? Watu wengi wanaaga dunia lakini wachache wanakumbukwa na ulimwengu huku wengine wakikumbukwa na familia zao tu. Kufanya kazi ni wajibu wa kila mtu lakini hakikisha unafurahia kazi uifanyayo ili iwasaidie wengi zaidi ya wewe pekee (oneself). Kwa kufanya hivyo utajenga ukuta imara kati yako na wanaokuzunguka na pengine zaidi za hapo kwa kuujumlisha ulimwengu. TENGENEZA HISTORIA SASA....

    Wednesday, June 15, 2016

    Maisha ya baadaye mali ya yule anayejiandaa leo.

    The Future belongs to those who prepare for it......

    Haya ni maneno ya mwanahistoria mmoja anayefahamika kwa jina la Malcom X.


    Ndugu, ukitaka maisha mazuri ya baadaye sharti ujiandae leo hii. Anza leo, usingoje kesho usiyokuwa na uhakika nayo. Watu wengi hupenda kusubiria kupata mtaji kamili ndipo waanze biashara. wengine husubiri wapate mtoto ndipo wajifunze kulea. wengine wanasubiri mitihani ikaribie ndipo waanze kusoma, wengine wanasubiri shida ndipo wamkumbuke Mungu, wengine hutaka kupunguza miili yao kwa afya njema lakini wanasema "nitaanza kesho au mwezi ujao au tarehe moja (nayo haifiki)". Tusiwe watu wa kusubiri....tuanze sasa. Chochote ulichonacho kiwe kingi au kidogo, anza nacho. UKITAKA MAZURI YA BAADAYE SHARTI UJIANDAE MAPEMA.

    J. A. Y

    Ninajijali, wewe je?

    Tuesday, June 14, 2016

    JINSI YA KUPIKA FUTARI YA MIHOGO NA SAMAKI


    MAHITAJI:
    • Mihogo
    • Nazi
    • Chumvi
    • Samaki
    • Limao/ndimu
    • Mafuta

    *Pilipili manga
    *Kitunguu swaumu
    *Tangawizi

    JINSI YA KUPIKA:
    • Mihogo

    Menya mihogo
    Kata kata vipande vidogo vidogo
    Bandika jikoni
    Acha kwenye moto kwa dakika kumi kama unatumia gesi
    Andaa nazi
    Mimina nazi kwenye mihogo ikiwa bado inachemka
    Tia chumvi kidogo
    Acha vitokote kwa dakika kumi nyingine ili nazi ichemke
    Bonyeza kwa mwiko uone kama imelainika 
    Kama imelainika epua, kama bado ongeza maji kidogo ili iive

    • Samaki

    Andaa samaki wako kwa kuwaparua na kuwaosha vizuri
    Wakate msitari kila upande
    Pakaa chumvi na limao/ndimu
    Pakaa viungo vingine kama pilipili manga, swaumu na tangawizi (ukipenda)
    Weka mafuta kwenye kikaangio
    Injika mafuta kwenye moto yachemke
    Kaanga samaki mpaka wawe na rangi ya kahawia
    Epua

    Waweza kuipamba sahani uliyopakulia chakula chako kwa kachumbari na limao/ndimu kwa ajili ya kuongeza ladha zaidi wakati wa kula.

    Nakutakia mlo mwema....

    Friday, May 27, 2016

    HUDUMA YA KWANZA

    Tumbo la kuhara

    Ni matumaini yangu hakuna mtu ambaye hajawahi kuumwa tumbo hata siku moja toka azaliwe. Lakini leo naongelea kuvurugwa kwa tumbo. Yawezekana ukawa umepata chakula mchnaganyiko ama vinywaji tofauti ambavyo vikasababisha kuvurugika kwa tumbo. Inawezekana ukawa umetoka sehemu moja kwenda nyingine yaani kubadilika kwa mazingira, hivyo kuhisi umevurugika tumbo. Lakini pia yawezekana ukawa unahofu sana kutokana na kusubiri matokeo fulani kama ya mtihani kimasomo ama majibu ya daktari ama ya usaili wa kazi. Yote haya na mengine mengi husababisha kuvurugika kwa tumbo na mara nyingi kupelekea kutaka kuhara (kuharisha).

    Mvurugiko huu wa tumbo humfanya mtu kukosa raha na hasa pale anapokuwa nje ya mazingira ya nyumbani ama sehemu iliyo karibu na huduma ya choo. Unachoweza kufanya ni kutafuta dawa ya kuzuia kuharisha kwenye maduka ya dawa yaliyoko karibu na wewe. LAKINI, si mara zote itawezekana kuwa hivyo, basi nini kifanyike unapokosa dawa hizo?

    Ukiwa nyumbani, chukua sukari na chumvi kisha chota chumvi kijiko kidogo cha chai nusu uweke kwenye kikombe na kiasi hicho hicho chota sukari uweke. Baada ya hapo changanya na maji kidogo sana ili kuepuka kupoteza ladha ya ukali dawa hiyo. Kwa kuwa uliweka kijiko kidogo nusu basi maji yaweke kiwango cha vijiko vikubwa vya kulia chakula vitano au sita. Koroga mchanganyiko wa chumvi na sukari kisha kunywa yote bila kuisikilizia. Tumbo litakata maumivu na dalili za kuhara mara moja. Na kama uliishaanza kuhara basi hali hiyo itaisha.

    Ukiwa nje ya mazingira ya nyumbani na hujapata msaada wowote wa chumvi na sukari ama dawa basi tafuta maji safi ya kunywa walau lita moja kisha vuta pumzi ndani na nje kwa nguvu kwa muda wa dakika tatu mpaka tano.