Thursday, April 21, 2016

Urefu wa kupindukia

Wewe ni mrefu? Ni mara ngapi umekutana na watu warefu? Ni nini kinafanya mtu awe mrefu? Fuatilia.....

Wanabiolojia wa molekuli (molecular biologists) wanaeleza kuwa tofauti ya urefu wa mtu na mtu kwa asilimia 60 mpaka 80 unatokana na maumbile huku asilimia 20 mpaka 40 unatokana na sababu za mazingira hasa lishe.  Urefu wa maumbile sana sana ni ule unaorithiwa hasa kutoka kwa mwanafamilia ama ndugu wa karibu.

Kila mmoja anahomoni za ukuaji (somatotropin) ambazo zinamsababisha kurefuka haraka ama taratibu. Utofauti huu ndio unaoleta utofauti katika urefu wa mtu na mtu.
Hizi homoni zina protini 191 zenye amino acid na uzito wa daltoni 22,124; na huzalishwa kwenye glandi iitwayo pituitary ambayo husambaza homini hizo mwilini kwa ajili ya ukuaji mara baada ya uzalishaji wake.

Wengi wetu tutakumbuka msemo wa wazazi kwa watoto wao wa "lala ukue" kama kumuhamasisha aende kulala hasa wakati wa mchana ambapo watoto wengi hupenda kuutumia kucheza. Inawezekana baadhi wa wazazi wanautumia kama mazoea lakini msemo huo unaukweli ndani yake.

Usambazaji wa homoni huchukua muda wa masaa matatu hadi matano lakini mtu hurefuka haraka ndani ya lisaa limoja tu akiwa amelala usingizi mzito. Hivyo ukuaji kutokea mara baada ya usambazaji wa homoni zinazohusika na ukuaji. Zikisambaa haraka na kwa wingi ndivyo mtu akuavyo mrefu zaidi kwa kipindi kifupi tu.

Homoni hizi hufanya kazi kwa ufanisi zaidi kwa watoto na vijana ambao wako katika kipindi cha ukuaji, na si kwa mtu mzima. Wazazi tuwashauri watoto wetu kupata usingizi wa kutosha ili kumsaidia kukua haraka.

Yamkini hawa ni wapenzi, pamoja na kuwepo kwa tofauti zao kiurefu bado wanaonekana kupendana. (picha kushoto)

Hawa nao ni marafiki, wao huchweza pamoja mpira wa kikapu. Wanaonekana kuwa wenye furaha sana ukiweka kando ukweli kuwa wamepishana sana urefu. (picha chini kulia)


Hivyo, kama wewe ni mrefu kuzidi wenzako usijione wa tofauti sana, kaa nao, cheza nao, furahi pamoja nao na wala usijitenge kwani furaha yako ni furaha ya jamii nzima.
Na kama wewe si mrefu usijishangae pia na wala usimtenge aliye mrefu zaidi yako.

Kinachofanya mtu awe mkubwa zaidi au mdogo zaidi ni sehemu ya mbele ya glandi ya pituitary iitwayo 'anterior pituitary'. Ikifanya kazi kupita kiwango humfanya mtu kuwa mrefu mno yaani 'giant' na vile vile inapofanya kazi chini ya kiwango basi mtu huwa mfupi zaidi yaani 'dwarf'.

Ewe kijana, unataka kuwa mrefu? Nawe mzazi, unataka mwanao arefuke vizuri? basi kama uko kwenye umri wa ukuaji bado unayo nafasi. Epukana na vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi (junk food). Pata lishe iliyobora kuisaidia glandi inayohusika na homoni za ukuaji kufanya kazi sahihi katika mwili wako. Hakikisha unapata usingizi wa kutosha ili kurahishisha somatotropin (homoni za ukuaji) kufanya mzunguko vizuri katika mfumo wake.


Kunywa maziwa ili upate calcium itakayokuimarishia mifupa yako. Urefu ukiambatana na mifupa legevu unaweza kupata matege lakini ukipata calcium basi unakuwa imara muda wote. Kula vyakula vyenye amino acid mfano samaki, mayai, mboga mboga kama mabilinganya na matunda kama karoti matikiti na maepo.

No comments:

Post a Comment