Friday, April 22, 2016

MoYo


Je, unaufahamu kuwa kila mwanadamu anapumua kwa msaada wa moyo? Na je, unafahamu kuwa moyo huo huo unaweza kumfanya mtu kuwa na furaha ama huzuni? 

Hii ni alama ambayo wengi huitumia kuashiria moyo na moyo huo basi unatumika kama ishara ya upendo. 
Moyo ni pampu inayosukuma damu kupitia mishipa ya damu. Kupitia mishipa hiyo damu husambazwa mwili mzima ili kukupatia hewa safi (oxygen). Tukiachana na maswala ya kibaiolojia, moyo unakazi ya kupenda.

Basi tuone upendo huo unaathiri vipi moyo na wewe kama binadamu unaukosea vipi moyo wako ama moyo wa mwingine. Jijali, mjali na mwenzio ili kuufurahisha moyo kwa afya zaidi. 



Huu ni moyo wa binadamu. 
Unapokuwa umezungukwa na watu wakupendao haijalishi ni upendo wa aina gani, moyo huwa na nguvu na hufanya kazi yake vizuri. Kila mmoja anapenda kupendwa, hata wababe huwa na wafuasi wao hata kama hawana upendo wa dhati.
Moyo wenye furaha. 
Moyo wenye nguvu

Moyo wenye furaha huimba ndani yetu pale tunapoongeza marafiki wapya. Moyo wenye furaha huupoza mwili tusikiapo baridi yaani tuwapo wapweke, kwa kukumbuka mema mengi yaliyopita. Inawezekana kabisa kwa wewe kujichangamsha bila kusubiri kuchangamshwa.

Moyo imara ni moyo wenye nguvu kwani unaweza kupigana na majaribu yote yanayotukumba katika maisha. Sisi sote tunapaswa kuwa na moyo wenye nguvu kwani pia ni rahisi kupingana na magonjwa tukianza na ugonjwa wa 'moyo' wenyewe.

Upendo wa nguvu
Upendo wa mahusiano ya kimapenzi ni upendo unaoleta hisia za kipekee. Kila mmoja anaweza kuuelezea ajuavyo yeye. LAKINI, maumivu ya kuachana kwa wapenzi hao yanaweza kuwa yanafanana kwani yote huumiza moyo.

Upendo unaolega lega
Afya ya mtu ni ya thamani, ni vema kutumia nafasi unayopata kwa mpenzi wako kumuonesha upendo na kupata upendo kutoka kwake. Kama unadhani hujaamua bado kujiingiza kwenye mahusiano, basi tafakari kabla ya kuchukua hatua. Ni vema kujiamini kwa ulifanyalo kuepukana na maumivu ya moyo. Kipindi tu unapojihusisha na mahusiano ya kimapenzi, fahamu kuwa unajifunga. 

Moyo uliofungwa kwa upendaye,
usiufungulie kwa wengine. 
Angalizo: Ili kuulinda moyo (wako/mwemzako) na maumivu zingatia haya:-
  • usiruhusu mtu kukuzoea haraka
  • usitoe siri zako 
  • usiseme udhaifu wako 
  • usijihakikishie mahusiano marefu (ingawa inapaswa kuwa hivyo)
  • usimchagulie mtu mpenzi
  • usimlazimishe mtu kukupenda
  • usijilazimishe kumpenda mtu
  • usimtumie mtu kama njia ya kumsahau aliyekuumiza
  • usiogope kumuambia unampenda (kama ndio mmeonana) bila kujali wewe ni ME au KE.
  • usipoteze muda mwingi kujifikiria juu ya jibu la kutoa 
  • usianzishe mahisiano mengine wakati uliyonayo sasa hayajaisha
  • usiwe mkimya sana wala mchangamfu kupita kiasi (utaboa)
  • usisubiri kutafutwa, anza pia (usitegee)
  • usingoje kusaidiwa, saidia pia (ushirikiano)
  • usiwe mkali sana ama mbabe kwa mwenzio
  • mkumbatie kwa muda mrefu kila upatapo nafasi (kumbato husaidia kuondoa huzuni kwa kiasi fulani lakini pia huzidisha ukaribu)
  • mpatie zawadi ndogo ndogo (mfanye atabasamu)
  • mchekeshe kwa vistori na michejo
  • muombe msamaha hata kama amekosa yeye
  • mwambie unampenda mara kwa mara
  • usijaribu mahusiano na mtu mwenye mahusiano
Ukipata mwenzako mshikilie sawa sawa
Ni bora kuumia kidole kitapona au kuvunjika kidole vingine vitafanya kazi lakini sio kuumia moyo sababu maumivu yake yaweza kuchukua miaka kuisha na kuvunjika kwa moyo ni ngumu kuutengeneza ukafanya kazi sawia.
Moyo usioweza
kufanya maamuzi
sahihi
Moyo ulionyong'onyea
na kudhoofika
Moyo
uliochanganyikiwa.
Hapa ndipo tunaposhauriwa kuwa na imani kwa kumuomba Mungu kwani yeye ndiye aliyekupa maisha. Jijali kwa kuepukana na athari hizo lakini pia, kama ikitokea ushaumizwa basi jitahidi kujishughulisha sana ili kupunguza mawazo. Kaa na watu watakupa mawazo tofauti usikae mwenyewe ukiwa mpweke kuepukana na mawazo potofu. Kemea roho ndani yako inayokusukuma kukata tamaa, kuchukia ama kujiua. Sali sana ukisikia hivyo kwa afya ya Roho na moyo pia.

Maumivu makali ya moyo 
Usiuzeeshe moyo wako kwa mambo usiyoyaweza. Usiukondeshe kwa kuupa mambo mengi usiyoweza kuyafuatilia na kuyafanya kwa ufanisi, usiufanye ukaelemewa. Ujali moyo wako kwa kujipenda na kuwa makini. Lakini kikubwa, usiutegemee moyo pekee katika mapenzi, shirikisha akili yako. Ni kwa kufanya hivyo, moyo utabaki kupenda tu huku mengine yakifanywa kwa utashi uliobarikiwa nao.

No comments:

Post a Comment