Thursday, August 18, 2016

KUMBATO NI TIBA

Kumbato mara nyingi hutumika tunaposalimiana ama kuagana kwa furaha na wapendwa wetu. Hii ni ishara ya furaha na mara nyingi huchukua sekunde chache sana kama 3 mpaka 6. 

Tunaposalimiana kwa mikono tunakuwa na umbali kiasi flani na ndiyo maana tunapokuwa makazini ama tukikutana na watu kwa mara ya kwanza tunapeana mikono kwa kuwa hatujawa karibu kiasi cha kuonyesha hisia zetu hasa za furaha kwao.

Kitendo cha kukumbatia ni sehemu mojawapo ya kudumisha upendo kati yetu na tuwapendao. Na kumbato hilo hilo hugeuka kuwa tiba hasa tunapotumia sekunde nyingi zaidi walau 20 na kuendelea.


Unapomkumbatia mtu ipasavyo, unakuwa na nafasi kubwa sana ya kuondoa ugonjwa, kutuliza hasira, kutuliza au kuondoa shauku, kutoa upweke, kupoteza huzuni na hata kupunguza na kuondoa kabisa msongo wa mawazo.
Tuangalie manufaa ya kumbato kwa undani wake:
  • Malezi yanayohusisha mguso wa kumbato hujenga hali ya uaminifu na hisia ya usalama. Hii husaidia kuleta mawasiliano ya wazi na yenye uaminifu.
  • Kumbato linaweza kuongeza kiwango cha Oxytocin papo hapo na kukuinulia hisia chanya. Nayo hutoa hisia ya upweke, kutengwa, shauku kali na hasira.
  • Kukumbatia kwa muda mrefu hunyanyua viwango vya Serotonin hivyo kuinua mudi ya kujenga furaha.
  • Kumbato huimarisha mfumo wa kinga hivyo kukulinda na magonjwa. Shinikizo la taratibu katika Sternum na chaji za hisia, hujenga na kufanya Solar Plexus Chakra kuwa hai hivyo kuchochea kongosho tezi, ambayo husimamia uzalishwaji wa seli nyeupe za damu mwilini. Solar Plexus Chakra ni msingi wa utu wetu, utambulisho wetu na u-sisi wetu.

  •  Unapokumbatia unalegeza mishipa. Hii huondoa mvutano mwilini mwako na kukuondolea maumivu kwa kuongeza mzunguko katika tishu laini hivyo kukupoza na kukupa tulizo.
  • Kumbato huweka usawa katika mfumo wa neva. Majibu ya mtu ya ngozi ya Galvanic katika kutoa na kupokea kumbato huonyesha mabadiliko ya nguvu katika ngozi. Athari ndani ya unyevu na umeme katika ngozi hupendekeza hali ya usawa zaidi katika mfumo wa neva.
  • Ni jambo linalotufundisha kutoa na kupokea. Ukikumbatiana na mtu au watu unapata thamani ya usawa ya kutoa na kupokea joto kama kutoa na kugawana. Inaelimisha juu ya upendo kwa wote wakumbatianao (wawili, watatu au kundi).
  • Kukumbatiana ni kama tafakari ya undani au kicheko cha furaha ambavyo kufdunza kusahau ama kupotezea yale yanayobugudhi, yanayokwaza au kuumiza na kujikita katika usasa yaani kuishi kwa wakati uliopo. 
  • Kumbato hukufanya ujisikie uko hai. Hukupa mzunguko wa mawazo mbalimbali yaliyo katika maumbo tofauti na kukuunganisha na moyo pamoja na pumzi yako.
  • Kumbato huletea hali ya kujiamini. Hali ambayo imekaa ndani yetu toka udogo wetu ambapo tumekuwa tukikumbatiwa na kubebwa kwa upendo na wapendwa wetu kama ndugu jamaa na marafiki. Hisia hizi zimekuwa ndani yetu kadiri tukuavyo hivyo kutujengea nguvu na uwezo wa kujipenda.
  • Kumbato la nguvu linalogusisha mioyo ya wawili wakumbatianao hufanya upendo kati yao kuwa maradufu hivyo kuweka uzio usioweza kuwatenganisha kirahisi kwani upendo ni dawa ya ajabu. 
  • Kumbato pia huimarisha saikolojia yetu na kuleta maendeleo ya miili yetu kwani hukufanya tulivu na mwenye afya ya roho na mwili pia.
  • Nguvu unayobadilishana na umkumbatiaye huwekezwa katika mahusiano yenu (mama na mwana, baba na mwana, marafiki, kaka na dada, wapenzi na kadhalika). Nguvu hiyo huleta hamasa ya uelewa baina yenu na mwisho kuwafanya mdumu.
  • Pia husaidia kunyoosha misuli ya nyuso, kuondoa mikunjo ya uzee pamoja na kufanya uzee uje taratibu ama kupunguza kasi ya uzee.
Varginia Satir ni mtaalamu anayeheshimika katika mambo ya familia. Yeye aliweza kufanya utafiti mdogo na kujiwekea msemo ambao sote tukiuzingatia tunaweza imarisha afya zetu kwa kiwango fulani. Anasema:

*Tunahitaji kumbato mara 4 kwa siku ili KUISHI
* Tunahitaji kumbato mara 8 ili KUREKEBISHIKA / KUIMARIKA
*Tunahitaji kumbato mara 12 ili KUKUA

Kwa wale wapendanao (wapenzi), kumbato ni chanzo kikubwa cha kuboresha mahusiano yenu  na tafiti nyingi zimeonyesha kuwa, wapenzi wanaokumbatiana sana hudumu kwenye mahusiano yao kwa muda mrefu.

Tibu maumivu yako sasa, tibu upweke na hali zote mbaya unazozipata kwa kupata kumbato. Anza kukumbatia watu zaidi kwa tiba rahisi zaidi.

Friday, July 22, 2016

Msukumo / motisha

Endelea kukimbia hata kama ni wa mwisho katika mashindano. Huwezi jua, yawezekama ukawa bingwa.

Ninawakummbusha ndugu zanguni kutokata tamaa maana muda unaokata tamaa unaweza kuwa ndio muda sahihi kabisa kwa wewe kupata mafanikio/ ukitakacho/ ulichoomba kwa muda mrefu/ kufikia ndoto zako na kadhalika.

Ukihisi kuacha usiache, kazana kwa kuwa umekaribia. Sote ni washindi kwa muda tofauti na kwa namna tofauti.

Thursday, July 21, 2016

Kila lililokamilika huanza kwa uamuzi wa kujaribu.


Msemo wa leo ni wa kutuhamasisha zaidi. Kila lililokamilika huanza kwa uamuzi wa kujaribu.

Chukua mfano huu mdogo. Umekaa kochini ukatamani maji ya kunywa lakini unaona uvivu kunyanyuka, hutapata maji. Kuna watu ndani unashindwa kuwaomba msaada wakuletee, hutapata maji. Umepata ila ni ya moto unahitaji ya baridi na huchukui uamuzi wowote, hutakata kiu yako.

Sasa, unataka kufanikisha mipango yako ambayo pengine hujaanza hata kujipanga, hutaikamilisha. Inatakiwa ifikie wakati ambapo utasimama hata kama umechoka au hujiwezi kufedha au kimwili. Anza safari huku ukiomuomba Mungu, naye atakuimarisha ukiwa njiani na utafika salama.

Fanya maamuzi haraka ya wapi uanze ama wapi upite na sio maamuzi ya kuendelea kusubiri. Bora ujaribu ushindwe kuliko usijaribu kumbe unajikosesha faida. Na ukijaribu ukashindwa usikate tamaa haraka, jaribu tena na tena mpaka utakapoona haiwezekani kabisa; ingawaje hakuna lisilowezekana kwa Mungu. Utachelewa lakini sio kushindwa.

Kazi kwako...

Wednesday, July 20, 2016

Onyesha heshima hata kwa watu wasiostahili; sio kwa muonekano wa tabia zao ila muonekano wa yako.


Maneno ya Dave Willis yanakumbushia utoaji wa heshima. Waswahili wanasema "heshima ni kitu cha bure" yaani huhitaji kulipia wala kugharamia chochote kuheshimu ama kuheshimiwa ila kujiheshimu na kutoa heshima hiyo kwa wengine wote hata kama hawastahili heshima yako.

Inakuwaje mtu hastahili heshima yako? Ni kwa sababu haonyeshi upendo kwako kama binadamu, sababu anakuona uko chini sana, sababu anakudharau, anakuona hufai kwake na katika maisha yake, sababu huna uwezo kifedha ama kifikra, sababu huwezi kufika alipofika, sababu hujampa alichotaka, hauna muonekano mzuri na mengine mengi.

Zipo sababu nyingi lakini pamoja na yote tunapaswa kukumbuka kuwa sote ni binadamu na tunakosea. Inawezekana tukapishana leo  lakini tukumbuke dunia huzunguka, binadamu pia. Tuheshimiane kwani hatujui ya kesho, inawezekana ukamheshimu mtu leo hata kama hastahili na kesho akawa msaada mkubwa tu kwako. Lakini tukijikweza leo, kesho tutaaibika.

Usimuhemu huyu ukamuacha yule ukidhani unakuwa mwema zaidi. Heshimu wote ili uonekane mwenye heshima.

AFRITRACUL




 Hivi ni vitu vya kiafrika kabisa. Vaa upendeze. Pendeza nasi AFRITRACUL kwa bei nzuri kabisa. Unaweza kutoa oda ya kitu ukitakacho ukatengenezewa. Jumla na reja reja unapata. Karibuni nyote.