Thursday, August 18, 2016

KUMBATO NI TIBA

Kumbato mara nyingi hutumika tunaposalimiana ama kuagana kwa furaha na wapendwa wetu. Hii ni ishara ya furaha na mara nyingi huchukua sekunde chache sana kama 3 mpaka 6. 

Tunaposalimiana kwa mikono tunakuwa na umbali kiasi flani na ndiyo maana tunapokuwa makazini ama tukikutana na watu kwa mara ya kwanza tunapeana mikono kwa kuwa hatujawa karibu kiasi cha kuonyesha hisia zetu hasa za furaha kwao.

Kitendo cha kukumbatia ni sehemu mojawapo ya kudumisha upendo kati yetu na tuwapendao. Na kumbato hilo hilo hugeuka kuwa tiba hasa tunapotumia sekunde nyingi zaidi walau 20 na kuendelea.


Unapomkumbatia mtu ipasavyo, unakuwa na nafasi kubwa sana ya kuondoa ugonjwa, kutuliza hasira, kutuliza au kuondoa shauku, kutoa upweke, kupoteza huzuni na hata kupunguza na kuondoa kabisa msongo wa mawazo.
Tuangalie manufaa ya kumbato kwa undani wake:
  • Malezi yanayohusisha mguso wa kumbato hujenga hali ya uaminifu na hisia ya usalama. Hii husaidia kuleta mawasiliano ya wazi na yenye uaminifu.
  • Kumbato linaweza kuongeza kiwango cha Oxytocin papo hapo na kukuinulia hisia chanya. Nayo hutoa hisia ya upweke, kutengwa, shauku kali na hasira.
  • Kukumbatia kwa muda mrefu hunyanyua viwango vya Serotonin hivyo kuinua mudi ya kujenga furaha.
  • Kumbato huimarisha mfumo wa kinga hivyo kukulinda na magonjwa. Shinikizo la taratibu katika Sternum na chaji za hisia, hujenga na kufanya Solar Plexus Chakra kuwa hai hivyo kuchochea kongosho tezi, ambayo husimamia uzalishwaji wa seli nyeupe za damu mwilini. Solar Plexus Chakra ni msingi wa utu wetu, utambulisho wetu na u-sisi wetu.

  •  Unapokumbatia unalegeza mishipa. Hii huondoa mvutano mwilini mwako na kukuondolea maumivu kwa kuongeza mzunguko katika tishu laini hivyo kukupoza na kukupa tulizo.
  • Kumbato huweka usawa katika mfumo wa neva. Majibu ya mtu ya ngozi ya Galvanic katika kutoa na kupokea kumbato huonyesha mabadiliko ya nguvu katika ngozi. Athari ndani ya unyevu na umeme katika ngozi hupendekeza hali ya usawa zaidi katika mfumo wa neva.
  • Ni jambo linalotufundisha kutoa na kupokea. Ukikumbatiana na mtu au watu unapata thamani ya usawa ya kutoa na kupokea joto kama kutoa na kugawana. Inaelimisha juu ya upendo kwa wote wakumbatianao (wawili, watatu au kundi).
  • Kukumbatiana ni kama tafakari ya undani au kicheko cha furaha ambavyo kufdunza kusahau ama kupotezea yale yanayobugudhi, yanayokwaza au kuumiza na kujikita katika usasa yaani kuishi kwa wakati uliopo. 
  • Kumbato hukufanya ujisikie uko hai. Hukupa mzunguko wa mawazo mbalimbali yaliyo katika maumbo tofauti na kukuunganisha na moyo pamoja na pumzi yako.
  • Kumbato huletea hali ya kujiamini. Hali ambayo imekaa ndani yetu toka udogo wetu ambapo tumekuwa tukikumbatiwa na kubebwa kwa upendo na wapendwa wetu kama ndugu jamaa na marafiki. Hisia hizi zimekuwa ndani yetu kadiri tukuavyo hivyo kutujengea nguvu na uwezo wa kujipenda.
  • Kumbato la nguvu linalogusisha mioyo ya wawili wakumbatianao hufanya upendo kati yao kuwa maradufu hivyo kuweka uzio usioweza kuwatenganisha kirahisi kwani upendo ni dawa ya ajabu. 
  • Kumbato pia huimarisha saikolojia yetu na kuleta maendeleo ya miili yetu kwani hukufanya tulivu na mwenye afya ya roho na mwili pia.
  • Nguvu unayobadilishana na umkumbatiaye huwekezwa katika mahusiano yenu (mama na mwana, baba na mwana, marafiki, kaka na dada, wapenzi na kadhalika). Nguvu hiyo huleta hamasa ya uelewa baina yenu na mwisho kuwafanya mdumu.
  • Pia husaidia kunyoosha misuli ya nyuso, kuondoa mikunjo ya uzee pamoja na kufanya uzee uje taratibu ama kupunguza kasi ya uzee.
Varginia Satir ni mtaalamu anayeheshimika katika mambo ya familia. Yeye aliweza kufanya utafiti mdogo na kujiwekea msemo ambao sote tukiuzingatia tunaweza imarisha afya zetu kwa kiwango fulani. Anasema:

*Tunahitaji kumbato mara 4 kwa siku ili KUISHI
* Tunahitaji kumbato mara 8 ili KUREKEBISHIKA / KUIMARIKA
*Tunahitaji kumbato mara 12 ili KUKUA

Kwa wale wapendanao (wapenzi), kumbato ni chanzo kikubwa cha kuboresha mahusiano yenu  na tafiti nyingi zimeonyesha kuwa, wapenzi wanaokumbatiana sana hudumu kwenye mahusiano yao kwa muda mrefu.

Tibu maumivu yako sasa, tibu upweke na hali zote mbaya unazozipata kwa kupata kumbato. Anza kukumbatia watu zaidi kwa tiba rahisi zaidi.