Friday, May 27, 2016

HUDUMA YA KWANZA

Tumbo la kuhara

Ni matumaini yangu hakuna mtu ambaye hajawahi kuumwa tumbo hata siku moja toka azaliwe. Lakini leo naongelea kuvurugwa kwa tumbo. Yawezekana ukawa umepata chakula mchnaganyiko ama vinywaji tofauti ambavyo vikasababisha kuvurugika kwa tumbo. Inawezekana ukawa umetoka sehemu moja kwenda nyingine yaani kubadilika kwa mazingira, hivyo kuhisi umevurugika tumbo. Lakini pia yawezekana ukawa unahofu sana kutokana na kusubiri matokeo fulani kama ya mtihani kimasomo ama majibu ya daktari ama ya usaili wa kazi. Yote haya na mengine mengi husababisha kuvurugika kwa tumbo na mara nyingi kupelekea kutaka kuhara (kuharisha).

Mvurugiko huu wa tumbo humfanya mtu kukosa raha na hasa pale anapokuwa nje ya mazingira ya nyumbani ama sehemu iliyo karibu na huduma ya choo. Unachoweza kufanya ni kutafuta dawa ya kuzuia kuharisha kwenye maduka ya dawa yaliyoko karibu na wewe. LAKINI, si mara zote itawezekana kuwa hivyo, basi nini kifanyike unapokosa dawa hizo?

Ukiwa nyumbani, chukua sukari na chumvi kisha chota chumvi kijiko kidogo cha chai nusu uweke kwenye kikombe na kiasi hicho hicho chota sukari uweke. Baada ya hapo changanya na maji kidogo sana ili kuepuka kupoteza ladha ya ukali dawa hiyo. Kwa kuwa uliweka kijiko kidogo nusu basi maji yaweke kiwango cha vijiko vikubwa vya kulia chakula vitano au sita. Koroga mchanganyiko wa chumvi na sukari kisha kunywa yote bila kuisikilizia. Tumbo litakata maumivu na dalili za kuhara mara moja. Na kama uliishaanza kuhara basi hali hiyo itaisha.

Ukiwa nje ya mazingira ya nyumbani na hujapata msaada wowote wa chumvi na sukari ama dawa basi tafuta maji safi ya kunywa walau lita moja kisha vuta pumzi ndani na nje kwa nguvu kwa muda wa dakika tatu mpaka tano.